• Toll Free: 0800110088
  • Box: 2932, Sinde Area - Mbeya Tanzania

Kuhakiki Utendaji wa Dira

Watumishi wa Mamlaka wakiwa katika zoezi la kupita nyumba kwa nyumba kuhakiki utendaji wa dira na kukusanya madeni ya ankara za maji.

Utiajia Saini Mkataba wa kutekeleza mradi wa Kiwira

Waziri wa Maji Jumaa Hamidu Aweso, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson, Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi pamoja na Mkuu wa Mkoa Mbeya Juma Zuberi Homera wakishuhudia zoezi la utiwaji saini mradi wa maji kutoka chanzo cha mto Kiwira

Uzinduzi wa Mradi wa Maji Shongo - Mbalizi

Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akizindua mradi mkubwa wa maji Shongo Mbalizi jijini Mbeya.

Mradi wa Kiwira

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi Mbeya (Kushoto) wakati wa hafla ya kutia saini Mkataba wa kuanza kazi ya kutekeleza mradi wa maji kutoka mto Kiwira

Maelezo ya Mradi

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera akipokea maelezo ya Mradi wa Maji Nzovwe-Isyesye alipotembelea miradi inayotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi Mbeya

Kutembelea wateja wakubwa

Mamlaka imetembelea Jeshi la Magereza ili kuwapa Elimu juu ya huduma za maji ikiwa ni pamoja na matumizi ya maji, bei za maji na jinsi ya kufanya malipo.

Kutunza vyanzo vya Maji

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi Mbeya akipanda miti katika maadhimisho ya Wiki ya Maji.

Usafi wa Mazingira

Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka wakifanya usafi wa Mazingira katika Wiki ya Maji.

Kutunza Vyanzo vya Maji

Maji ni Uhai, tunza vyanzo vya Maji

KARIBU MAMLAKA YA MAJISAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MBEYA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (Mbeya UWSA) ni miongoni mwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanzania Bara. Mamlaka ilianzishwa mwaka 1998 kwa Sheria Na. 8 ya 'Water Works Act Cap 272' ya mwaka 1997, iliyofanyiwa marekebisho na Sheria Na.12 ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009. Mamlaka ya Majisafi Mbeya imepatiwa daraja "A".

Mamlaka ya daraja "A" inawajibika kugharamia shughuli za uendeshaji, matengenezo, mishahara na kuchangia asilimia 15% ya mapato yake kwenye shughuli za maendeleo. Mamlaka ina dhamana ya kutoa huduma bora ya majisafi pamoja na usafi wa mazingira kwa wakazi waishio Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi iliyopo Kusini Magharibi mwa Tanzania. Miji hii inakadiriwa kuwa na wakazi wapatao 630,000 (Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022).

DIRA (VISION)

Kuwa mamlaka bora kwa kutoa huduma bora na endelevu ya majisafi na usafi wa mazingira ifikapo 2025.

DHIMA (MISSION)

Kutoa huduma bora na endelevu ya majisafi na usafi wa mazingira kwa wakazi wa Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi kwa bei himilivu.

KAULIMBIU (SLOGAN)

'Maji ni Uhai'

MISINGI YA UTENDAJI (CORE VALUES)
  • Wateja Kwanza
  • Watumishi ni Rasilimali namba moja ya Mamlaka
  • Kuwajibika kwa jamii inayotuzunguka
  • Nidhamu katika matumizi ya Fedha
  • Watumishi kufanyakazi kwa pamoja na kujituma.
  • Wafanyakazi kuhimizwa kujifunza na kubadilishana maarifa.
MACHAPISHO NA FOMU

MKURUGENZI MTENDAJI CPA. Gilbert Kayange


KURIPOTI MIVUJO NA WIZI WA MAJI

Ili kuripot mvujo wa maji (Mfano: bomba kupasuka n.k), kuripoti wizi wa maji au uharibifu wowote wa miundombinu ya maji, tafadhali piga simu ya Ofisi namba: 0800110088 bure.

GALLERY


Bonyeza hapa kwa picha zaidi

Habari Mpya

Matukio Kwa Picha

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AIPONGEZA SEKTA YA MAJI MBEYA KWA UTUNZAJI WA VYANZO VYA MAJI

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu Abdala Shaibu Karim, apongeza jitihada za uhifadhi wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji Jijini Mbeya baada ya kutembelea chanzo cha maji Ivumwe na kujionea namna Sekta ya Maji Mbeya inavyoshirikiana na wananchi.

MAADHIMISHO YA KILELE CHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya yashiriki maadhimisho ya kilele cha Siku ya Mazingira duniani. Maadhimisho haya yaliyobeba Kaulimbiu ''PUNGUZA UCHAFUZI WA MAZINGIRA UNAOTOKANA NA TAKA ZA PLASTIKI" yamehitishwa leo, tarehe 05 Mei, 2023 kwa kufanya usafi katika Soko la Sido na Mitaro ya barabarani.

Mkurugenzi Mtendaji akiongea na watumishi

Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya CPA. Gilbert Kayange, amepata nafasi ya kuongea na watumishi katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi za Mamlaka. Aidha Mkurugenzi amewaeleza watumishi malengo ya Mamlaka pamoja na hali ya huduma ya Maji kwa jiji la Mbeya, pia aliwasihi watumishi kufanya kazi kwa uadilifu,bidii na weledi.