![]() |
Ili upate kuunganishwa na huduma ya majisafi/majitaka, Mteja atapaswa kujaza fomu ya Mamlaka ya maji kwa njia ya kielektroniki inayopatikana kwa kiungo cha huduma.maji.gov.go.tz. Mteja anahitajika kuwa na viambatisho vifuatavyo katika mfumo wa nakala line (softcopy - PDF format).
Mteja anaweza kulipia ankara ya maji kwa mawakala wote wa Benki za Posta, NMB, NBC, na CRDB na Kupitia mitandao ya simu kwa huduma za MPESA, AIRTEL MONEY, TTCL PESA, EASY PESA, na HALOPESA. Ili kuweza kufanya malipo, ni lazima kuwa na Namba ya Malipo (Control Number) ina tarakimu kumi na mbili (Mfano: 994550451254). Kulipa kwa simu fuata hatua hizi:-
Ikitokea mteja hapati bili ya maji kwa njia ya meseji itakua ni tatizo la mtandao (network) hivyo mteja naombwa kuangalia bili yake kwa kuingia kwenye tovuti ya mamlaka kubonyeza kwenye menyu ya ankara na kufuata maelekezo. Au anaweza piga simu ya bure (0800110088) na kuuliza ankara yake. Au kwa bonyeza hapa Angalia ankara. Au mteja anaweza tumia simu yake kwa kubonyeza *152*00# na kufuata maelekezo. Au kwa kupakua 'App' ya GePG Tanzania, chagua maji (water) kisha chagua angalia bili yako.
Dira inashindwa kusomwa na wasomaji kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kwamba dira inakua imefungiwa ndani ya uzio wa nyumba ya mteja. Kwa kawaida msoma dira akisha soma ujumbe mfupi (sms) unatumwa kwa mteja kumjulisha juu ya usomaji kwa mwezi husika. Ikiwa msomaji dira wa Mamlaka hajafika kusoma kuanzia tarehe 01 hadi 15 ya kila mwezi, tafadhali ripoti suala hili mara moja katika ofisi za Mamlaka kwa kupiga simu ya bure (0800110088) ili kuepuka bili kua kubwa wakati itakaposomwa miezi inayofuata.
Ikiwa mteja amekosea kufanya malipo ya maji na kwamba pesa imeenda kwa mteja mwingine, atapaswa kufika ofisini kueleza suala hili na ikithibitika kwamba ni kweli alifanya malipo kimakosa. Ataelekezwa kuandika barua ili kuomba fedha aliyolipa iingizwe kwenye account yake sahihi. Hata hivyo Mamlaka inasisitiza wateja kuwa makini sana wanapofanya malipo kwa kuangalia jina linalotokea wakati analipa kwa wakala au mtandao wa simu.
Bili inaeza kua kubwa katika mwezi Fulani kuliko miezi mingine kwa sababu zifuatazo:-
Ikiwa mteja atasitishiwa huduma ya maji kwa sababu yoyote ile, huduma itarudishwa ndani ya siku 1 hadi 2 za kazi mara baada ya kulipia gharama za kurejesha huduma.