• Toll Free: 0800110088
  • Box: 2932, Sinde Area - Mbeya Tanzania

ZIARA YA WAZIRI MHE. JUMAA AWESO KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MRADI KUTOKA CHANZO CHA MTO KIWIRA

Ziara ya Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso kukagua utekelezaji wa mradi wa maji kutoka chanzo cha Mto Kiwira tarehe 23/07/2025.Mradi wa maji toka chanzo cha mto Kiwira ni mradi wa kimkakati unaolenga kumaliza changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Mbeya na maeneo ya jirani kwani utazalisha maji lita milioni 117 kwa siku.

UJENZI WA TENKI LA FOREST

Ujenzi wa tenki katika eneo la forest ukiendelea. Hii ni hatua katika kazi inayendelea ya ujenzi wa mradi wa maji kutoka chanzo cha mto Kiwira

Kilele cha Wiki ya Huduma kwa Mteja

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya imekabidhi mashuka 100 yenye gharama ya sh. 2,400,000 kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya, ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa mteja

Uzinduzi wa Mradi wa Maji Shongo - Mbalizi

Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan akizindua mradi mkubwa wa maji Shongo Mbalizi jijini Mbeya.

Mradi wa Kiwira

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi Mbeya (Kushoto) wakati wa hafla ya kutia saini Mkataba wa kuanza kazi ya kutekeleza mradi wa maji kutoka mto Kiwira

Kutembelea wateja wakubwa

Mamlaka imetembelea Jeshi la Magereza ili kuwapa Elimu juu ya huduma za maji ikiwa ni pamoja na matumizi ya maji, bei za maji na jinsi ya kufanya malipo.

Kutunza vyanzo vya Maji

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi Mbeya akipanda miti katika maadhimisho ya Wiki ya Maji.

Usafi wa Mazingira

Baadhi ya Watumishi wa Mamlaka wakifanya usafi wa Mazingira katika Wiki ya Maji.

Kutunza Vyanzo vya Maji

Maji ni Uhai, tunza vyanzo vya Maji

KARIBU MAMLAKA YA MAJISAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MBEYA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (Mbeya UWSA) ni miongoni mwa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanzania Bara. Mamlaka ilianzishwa mwaka 1998 kwa Sheria Na. 8 ya 'Water Works Act Cap 272' ya mwaka 1997, iliyofanyiwa marekebisho na Sheria Na.12 ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009. Mamlaka ya Majisafi Mbeya imepatiwa daraja "A".

Mamlaka ya daraja "A" inawajibika kugharamia shughuli za uendeshaji, matengenezo, mishahara na kuchangia asilimia 15% ya mapato yake kwenye shughuli za maendeleo. Mamlaka ina dhamana ya kutoa huduma bora ya majisafi pamoja na usafi wa mazingira kwa wakazi waishio Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi iliyopo Kusini Magharibi mwa Tanzania. Miji hii inakadiriwa kuwa na wakazi wapatao 630,000 (Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022).

DIRA (VISION)

Kuwa mamlaka bora kwa kutoa huduma bora na endelevu ya majisafi na usafi wa mazingira ifikapo 2025.

DHIMA (MISSION)

Kutoa huduma bora na endelevu ya majisafi na usafi wa mazingira kwa wakazi wa Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi kwa bei himilivu.

KAULIMBIU (SLOGAN)

'Maji ni Uhai'

MISINGI YA UTENDAJI (CORE VALUES)
  • Wateja Kwanza
  • Watumishi ni Rasilimali namba moja ya Mamlaka
  • Kuwajibika kwa jamii inayotuzunguka
  • Nidhamu katika matumizi ya Fedha
  • Watumishi kufanyakazi kwa pamoja na kujituma.
  • Wafanyakazi kuhimizwa kujifunza na kubadilishana maarifa.
MACHAPISHO NA FOMU

MKURUGENZI MTENDAJI CPA. Gilbert Kayange


KURIPOTI MIVUJO NA WIZI WA MAJI

Ili kuripot mvujo wa maji (Mfano: bomba kupasuka n.k), kuripoti wizi wa maji au uharibifu wowote wa miundombinu ya maji, tafadhali piga simu ya Ofisi namba: 0800110088 bure.

GALLERY


Bonyeza hapa kwa picha zaidi

Habari Mpya

Matukio Kwa Picha

BOMBA ZA MAJI ZA KIPENYO CHA MILIMITA 1,200 YATUA MBEYA KWA AJILI YA KUTEKELEZA MRADI WA MAJI WA MTO KIWIRA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya imepokea sehemu ya bomba ya utekelezaji wa mradi wa Maji toka chanzo cha mto Kiwira. Bomba hizo zimepokelewa leo tarehe 18/04/2025, ambapo mgeni rasmi wa tukio hilo alikua ni Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Mabunge duniani. Dkt Tulia amemtaka Mkandarasi wa mradi kutekeleza mradi kwa kuzingatia viwango na kukamilisha mradi ndani ya muda uliopangwa.

NAIBU WAZIRI WA MAJI ATEMBELEA MRADI WA MAJI KUTOKA CHANZO CHA MTO KIWIRA

Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mwethew alipotembelea na kukagua maendeleo ya utekelezaji wa wa mradi wa maji kutoka chanzo cha Mto Kiwira. Akiwa katika ziara hiyo ameagiza wataalamu washauri kuongeza kazi ya utekelezaji ili kuwezesha mradi huo kukamilika kwa wakati

MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI DUNIANI

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya, imeendelea kufanya maadhiisho ya Wiki ya Maji Duniani kwa kufanya usafi katika chanzo cha maji Nzovwe . Mbeya UWSA kwa kushirikiana na Watumishi wa Bonde la Ziwa Rukwa, RUWASA na Wananchi wamefanya usafi sambamba na kutoa elimu ya utunzaji wa vyanzo vya maji kwa wakazi wa eneo hilo.